Skip to main content
PROGRAM INAANZA JUNI 06 2026

Start Point Academy, Mwanao atajenga ujuzi wa maisha kwa mikono yake mwenyewe

Fikiri kwa makini. Tatua tatizo. Rudia.

Start Point Academy ni nini?

Ni programu ya wikiendi kwa watoto wa shule ya msingi inayowasaidia kutumia kompyuta, internet, na AI kutengeneza suluhisho kwa matatizo halisi sambamba na shule yao

Si tuition

Mtoto hafundishwi kukariri. Anafundishwa kuona tatizo, kupanga hatua, kujaribu, na kurekebisha mpaka apate suluhisho.

Kujifunza kwa vitendo

Watoto wanatengeneza programu na mifumo halisi kwaajili ya kutatua matatizo katika jamii

Sambamba na shule

Program inafanyika wikiendi bila kuingilia ratiba ya shule, mitihani, au masomo ya kawaida. Ratiba maalum hutolewa kwa vipindi vya likizo.

Mtoto wako atajifunza nini hapa?

Haya ndiyo mambo ya msingi tunayomjengea mtoto wako mapema ili aweze kua tayari kukabiliana na mazingira halisi

Kutatua matatizo

Anaanza kuona changamoto na kufikiria jinsi ya kuitatua, si kuikwepa.

Kufikiri kwa kimantiki

Anajifunza kuvunja tatizo kwa hatua na kupanga suluhisho kwa mpangilio.

Kuprogram kompyuta

Anatumia kompyuta kutengeneza kitu kinachofanya kazi, si kuitumia kwa burudani tu.

Kushirikiana na wengine

Anajenga tabia ya kusikiliza, kushirikiana, na kueleza wazo lake kwa wengine.

Kujenga miradi

Mwisho wake mtoto ana kitu halisi cha kuonyesha, si hadithi tu ya alichosoma.

Kwa nini hii ni muhimu sasa?

Watoto wa leo wanahitaji zaidi ya kukariri. Wanahitaji ubunifu, kufikiri kwa kina, na uwezo wa kutumia teknolojia kutatua matatizo ya kweli.

Sera ya Elimu

Elimu ya Msingi inasisitiza ubunifu, kudadisi, kufikiri kiyakinifu, na kutatua matatizo. SPA inaleta hayo kwa vitendo.

Dira 2050

Taifa linahitaji watoto wenye msingi wa sayansi, teknolojia, uhandisi, hisabati, na ujuzi wa kidijitali kwa uchumi wa baadaye.

Kesho ya mtoto wako

Tunataka mtoto ajifunze kutumia kompyuta, internet, na AI kama zana za kazi halisi, si kwa kuperuzi na burudani tu.

Mtoto anajifunza kwa kufanya

Tunamtoa mtoto kwenye kusikiliza tu na kumpeleka kwenye kujenga, kujaribu, na kuonyesha kile alichotengeneza.

01

Anaanza na tatizo la shule

Mfano kwenye hesabu, Kiingereza, au kujipima kabla ya mtihani.

02

Anajenga suluhisho

Anaweza kutengeneza programu ya hesabu, mchezo wa msamiati, au quiz ya kujipima.

03

Anatumia AI kama kifaa cha kazi

Anajifunza kuitumia AI kama msaidizi wa kujenga kazi, si kama sehemu ya kupoteza muda

04

Anapanua mpaka nyumbani na jamii

Baadaye anaweza kujenga mfumo wa biashara ya familia au project ya kutatua changamoto ya jamii.

Kwa nini uamini Start Point Academy?

Start Point Academy si shule mpya na si tuition. Ni njia ya kumsaidia mtoto kujenga ujuzi wa baadaye bila kuacha msingi wake wa shule.

  • Sio tuition ya masomo ya darasani
  • Inafanya kazi sambamba na shule ya mtoto wako
  • Haiingilii ratiba ya shule, NECTA, mitihani, au matukio ya shule
  • Mtoto anajifunza kutumia teknolojia kwa tija, si burudani tu
  • Unapata kuona maendeleo kupitia kazi halisi anayojenga
Angalia Programu Kamili
Bila mwelekeo huu
  • Teknolojia inabaki kwa kuperuzi na burudani tu
  • Mtoto hutumia kompyuta bila kujua kuitumia kutatua tatizo
  • Karatasi na cheti pekee ndivyo vinaonekana
  • Uwezo wa mtoto kujenga kitu halisi hauonekani mapema
Kwa Start Point
  • Mtoto anajenga project halisi
  • Anatumia teknolojia kama suluhisho, si burudani tu
  • Anajifunza kueleza kazi yake kwa ujasiri
  • Anaanza kuona uwezo wake wa kujitegemea baadaye

Maelezo ya programu

  • Usajili: Unaendelea sasa
  • Ratiba: Wikiendi
  • Washiriki: Watoto Shule ya msingi
  • Mahali:Goba, Goba Mpakani
  • Ada: Tsh 100,000 kwa mwezi

Kwa nini uanze sasa?

Ili aanze kuona teknolojia kama fursa, si burudani tu

  • Mtoto anaanza kujenga kujiamini mapema
  • Atumie muda wake kwa tija
  • Ajenge msingi wa ubunifu na uchambuzi
  • Punguzo la 20% kwa watoto 16 wa kwanza.

Program inaongozwa na watu wenye uzoefu

Tunajenga program hii juu ya uzoefu wa teknolojia, elimu, na mbinu za Project Based Learning pamoja na Computational Thinking.

Mwanzilishi

Edgar Mlowe — ICT & AI expert, mwenye uzoefu wa takribani miaka 10 World Bank na miaka 5+ ya software consultancy na kampuni za Marekani.

Mkufunzi Mkuu

Nimrod Rutora — miaka 10 kwenye software industry, Lead Product Designer wa Silabu, kampuni kubwa ya elimu-mtandao Tanzania.

Methodology

Program imejengwa juu ya Project Based Learning na Computational Thinking ili mtoto ajifunze kwa kufanya, kujaribu, na kurekebisha.

Mpe mtoto wako nafasi ya kujenga uwezo wa kesho leo

Nafasi ni chache. Anza sasa kumsaidia kutumia teknolojia, AI, na ubunifu kutatua matatizo halisi na kujenga msingi wa maisha yake ya baadaye.

Jiunge →